Malaika alikuja asubuhi hii na kunipeleka Purgatori ili kusaidia Roho Takatifu. Tulipokuwa tunatoka pale, Malaika na mimi tulitembea kupanda mlima na kukutana na nguzo ndogo nyeupe. Tuliketi chini, na pamoja nasi walikuwepo wanawake wachache watakatifu.
Malaika alisema, “Valentina, inua macho yako juu.”
Nilivunua macho yangu juu na kuona Mbingu ikifunguka. Nilishuhudia vitu vikiandaliwa kisha vikashuka chini.
Malaika alisema, “Toa mkono wako.”
Nilipotoa mkono wangu, niliona kifurushi kikubwa cheupe kikishuka, kikiwa na msalaba wa bluu juu yake.
Malaika alisema, “Mungu Baba amekutumia kifurushi.” Nilifikiri labda Mungu Baba alikuwa akinitumia kitu kwa ajili ya mguu wangu, kwa sababu nilikuwa nikiuliza Ni lini Ataponyapo.
Kile kifurushi kikubwa sana kilitua kwenye mkono wangu uliokuwa umeinuliwa. Kilikuwa chepesi sana na kimefungwa katika karatasi laini nyeupe. Niliweka chini na kufikiri: Oh, msalaba wa bluu ni rangi ya Mama Mtakatifu. Msalaba huo wa bluu ulikuwa mpana kabisa ukiwa na urembo wa dhahabu.
Sikuifungua mara moja. Wote waliniuliza, “Hutafungua kuona ni nini?”
Hatimaye, nilifungua kifurushi kile na kupata chupa ndogo ya kahawia ya mraba ikiwa na kitu ndani yake. Niliacha karatasi ya kufungia na kuchukua ile chupa nami.
Waliuliza, “Kuna nini ndani yake?”
Nilipofungua chupa ile na kuangalia ndani, niliona rice bubbles pamoja na maziwa!
Sote tulicheka. Mungu Baba alikuwa amefanya utani kidogo nami.
Nilisema, “Hivyo ndivyo itakavyokuwa.”
“Lakini hiyo inatoka Mbinguni, kwa hivyo ni ya thamani sana. Mungu Baba alikuwa amekufanyia utani kidogo ili kukuchangamsha,” walisema.
Kisha niliendelea kutembea na Malaika. Tulipopinda kona, ghafla tulikutana na watu wawili wakubwa, mwanamume na mwanamke wenye rangi ya angavu ya ngozi, wakiwa wamevalia mavazi marefu meupe yenye vifuniko vya rangi ya beige. Walikuwa zaidi ya mita mbili kimo. Nikiwa nimesimama karibu nao, nilijihisi mdogo sana na nikawa na uoga. Walinitazama lakini hawakusema kitu, na wakapita wakiwa wameshikana mikono. Nilipogeuka nyuma, niliona wote wawili walikuwa na nywele nzuri ndefu, za rangi ya kahawia iliyopauka (ash blonde) na zinazong'aa.
“Wao ni warefu sana,” nilimwambia Malaika.
Malaika alieleza, “Valentina, je, unajua kwamba katika nyakati za kale sana kulikuwa na watu wakubwa wanaoishi duniani zamani za kale sana? Baadhi yao walikuwa wema na wengine hawakuwa wema. Baada ya karne nyingi, watu wakawa wadogo zaidi.”